Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Jaji afuta sheria ya uvaaji barakoa kwenye vyombo vya usafiri Marekani
Kimataifa

Jaji afuta sheria ya uvaaji barakoa kwenye vyombo vya usafiri Marekani

People wearing face masks on the London Underground, as the first case of coronavirus has been confirmed in Wales and two more were identified in England - bringing the total number in the UK to 19.
Spread the love

JAJI wa Mahakama moja katika jimbo la Florida nchini Marekani ameiondoa sheria ya uvaaji barakoa katika vyombo vyote vya usafiri nchini humo.

Jaji Kathryn Kimball Mizelle amesema kwamba sheria hiyo ya kuzuia maambukizi ya virusi vya corona ni kinyume cha sheria. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Jaji huyo aliyetoa uamuzi huo amesema amri ya kuvaa barakoa iliyotolewa na Mamlaka ya afya nchini humo (CDC) ilivuka mamlaka yake.

Uamuzi wa Jaji huyo unaenda kinyume na agizo la Rais wa Marekani, Joe Biden aliyesisitiza na kukazia amri hiyo ya CDC ili kukabiliana na janga la maambukizi ya virusi hivyo vya Corona.

Wamarekani walikuwa wanatakiwa kuvaa barakoa wanapokuwa kwenye ndege, treni na mabasi. Amri hiyo ilikuwa imeongezwa hadi mwezi Mei.

Hata hivyo, Ikulu ya White House na wizara ya haki zinaweza kukata rufaa kutokana na uamuzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!