BALOZI Mstaafu Dk. Wilbroad Slaa amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan atokeo hadharani atoke hadharani na kutoa kauli ili kuliokoa Taifa katika janga lililoibuka kwenye mkanganyiko wa mkataba wa uwekezaji kwenye bandari ya Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Dk. Slaa amesema Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa alisaini mkataba huo kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai kupitia kampuni ya DP World kwa kibali cha Rais Samia na mamlaka yake ambayo yameliingiza Taifa katika msiba mkubwa.
Akizungumza leo katika mkutano ulioandaliwa na Chadema kwa kushirikiana na Sauti ya Watanzania anayoongoza, Dk. Slaa amesema anaomba hivyo kwa sababu nchi ipo kwenye kilio.
“Hili la bandari mama nakuomba wewe ndiye uliyeshuhudia uwekaji saini wa Mkataba wa makubaliano (MOU) kati ya TPA na DP World hajawahi kutokea Rais anashuhudia tukio la aina hiyo.,
‘Pili nakuomba wewe uliweka saini power off attorney ukimruhusu Mbarawa asaini mikataba kati ya Tanzania na Dubai. Mbarawa alifanya kwa kibali chako kwa mamlaka yako umeingiza Taifa katika msiba mkubwa, toka hadharani kwa kauli… Rais Tanzania hakuna mwingine ni wewe toka utuokoe katika janga hili.
“Mwisho tumeingia kwenye haya kwa sababu ya katiba mbovu, kama isingekuwa mbovu wabunge kule Dodoma wasingefanya kiini macho walichofanya tarehe 10,” amesema Dk. Slaa.
Aidha, Dk. Slaa amemuomba Rais Samia kuwaandalia mazingira ya upatikanaji wa Katiba mpya na si kuwaandalia Katiba mpya kwani katiba hiyo ikipatikana ataongoza Taifa vizuri.
Leave a comment