Thursday , 9 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya DC Mpanda aagiza maji ya visima yapimwe kudhibiti kipindupindu
Afya

DC Mpanda aagiza maji ya visima yapimwe kudhibiti kipindupindu

Spread the love

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Jamila Yusuf ameziagiza mamlaka za afya na maji kushirikiana ili kuainisha idadi ya visima vilivyopo ndani ya wilaya hiyo na kuvipima kubaini maji ya visima hivyo yana usalama kiasi gani kwa matumizi ya binadamu. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Mkuu huyo wa wilaya ametoa maagizo hayo leo Ijumaa  katika kikao kazi maalum cha kuweka mikakati ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko hususani kipindupindu.

Amesema kila kaya inatakiwa kuzingatia suala la usafi wa mazingira, ikiwemo kunawa maji tiririka sanjari na kuwataka watumishi kuanzia ngazi ya serikali ya mtaa kuweka nguvu kazi katika kutunza mazingira, hiyo ikiwa ni njia mojawapo ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko.

Amewataka maofisa afya kufanya ukaguzi katika maeneo ya kutolea huduma ya chakula, stendi za mabasi na maeneo mengine yanayohusisha mkusanyiko wa watu, ikiwemo maeneo ya mabucha ili kuhakikisha udhibiti unaimarishwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!