Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CUF: ACT inakurupuka kujitoa SUK
Habari za Siasa

CUF: ACT inakurupuka kujitoa SUK

Maftaha Nachuma
Spread the love

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Maftaha Nachuma amesema kuwa Serikali ya umoja wa Kitaifa (SUK)-imetokana na maridhiano ya chama chao (CUF) na Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivyo Chama cha ACT-Wazalendo hakijui misingi yake ndio maana kinakurupuka kutaka kujitoa. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Nachuma ameyasema hayo jana tarehe 14 Machi 2024, wakati akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam na kueleza kuwa SUK haikuundwa kukinufaisha chama cha siasa isipokuwa imeanzishwa kwa maslahi ya wananchi wa Zanzibar.

” “Hakuna chama kilichopitia magumu kama Chama cha Wanachi -CUF, sisi ndio chama ambacho watu wake wengi waliuawa mwaka 2001 hadi Rais mstaafu Hayati Benjamini Mkapa akaelezea kujutia kwa mauaji hayo ndio maana nasema hawa wanaojitoa SUK hawajui misingi ya SUK,” amesema Nachuma.

Amesema kuwa msingi wa kuundwa kwa serikali ya umoja unatokana na kuchoshwa na matukio ya umwagaji damu za wanachi na kuunganisha mawazo ya Wazanzibar wote kwenye serikali.

“Tunafahamu bado kuna matatizo ndani ya Serikali ya CCM lakini sio suala la kujitoa kwenye SUK kwa sababu rahisi rahisi tu” amesema Nachuma.

1 Comment

  • Nachuma, umeongea. Tunashangaa huyu ACT Makamu wa Rais, baada ya kwenda mbele anaturudisha kusiko.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!