Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa COVID-19: Prof. Lipumba ‘watu wana hofu’
Habari za SiasaTangulizi

COVID-19: Prof. Lipumba ‘watu wana hofu’

Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF
Spread the love

 

PROFESA Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) amesema, wataalamu na wanasayansi Tanzania wamekuwa na hofu ya kueleza hali halisi kuhusu maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19) nchini. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Buguruni jijini Dar es Salaam, leo tarehe 7 Machi 2021 amesema, serikali itumie wanasayansi kukabili virusi vya corona.

“Hasa kwenye magazeti ya nje, watu wanaomba kutotajwa majina yao kutokana na woga wa kuingia matatani.

“Watu wana hofu, wanamashaka, wanaogopa. Tuiondoe hii hofu. Madaktari na wanasayansi waweze kufanya utafiti bila woga,” amesema.

Prof. Lipumba ameishauri serikali kushirikiana na mataifa mengine duniani ili kupata chanjo hiyo.

“Tunatoa wito kwa serikali kufanya utaratibu kwa kuwatumia wataalamu wa afya kufanyia uchunguzi chanjo za corona, hatimaye majibu ya wataalamu na ndio yaongoze uamuzi juu ya kutumia chanjo hizo.

“Tushirikiane na taasisi za kimataifa, tutumie wataalamu na tuwasikilize,” amesema Prof. Lipumba.

Tayari viongozi mbalimbali wa kiroho wamewataka waumini wao kuchukua tahadhari dhidi ya corona.

Hata hivyo, serikali imesisitiza Watanzania kuendelea kuchukua hatua za kujikinga na virusi hivyo.

Na kuwa, miongoni mwa hatua muhimu ni pamoja na kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka.

2 Comments

  • Naomba wahusika wanielimisha
    Wasafiri wanaotoka nje ya nchi (wakiwemo watalii) wanapimwa Corona kwa garama ya dola 100. Je wakionekana wameambukizwa na virusi vya Corona ndege inawakubali? Kama la, je watabaki nchini na watapatiwa matibabu? Ufukizaji au madawa ya wazungu?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!