Saturday , 11 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM wawarudisha Waitara, Kalanga
Habari za Siasa

CCM wawarudisha Waitara, Kalanga

Mwita Waitara, Naibu wa Waziri wa TAMISEMI
Spread the love

KAMATI Kuu Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM imeteuwa wagombea watatu watakaokiwakilisha chama hicho katika uchaguzi mdogo wa ubunge. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Kamati hiyo iliyoketi leo tarehe 14 Agosti, 2018 jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dk. John Magufuli, imemteuwa Julius Kalanga aliyekuwa Mbunge wa Monduli kupitia Chadema, kugombea tena kwenye jimbo hilo.

Pia, imemteua Mwita Waitara aliyekuwa Mbunge wa Ukonga kupitia Chadema, kugombea tena kwenye jimbo hilo kupitia CCM. Vilevile, imemteua Timotheo Mzava kugombea katika jimbo la Korogwe Vijijini.

Waitara na Kalanga hivi karibuni walijivua uanachama wa Chadema pamoja na ubunge na kuhamia CCM, chama hicho kimewapitisha tena kugombea kwenye majimbo yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina awavaa mawaziri wanaompelekea majungu Rais Samia

Spread the loveMBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amewataka baadhi ya mawaziri...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

error: Content is protected !!