RIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2022/2023 imbeinisha kuwa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania ilitoa hati za ugawaji wa maeneo ya uwindaji (vyeti namba TAWA.0003, TAWA.0004 na TAWA.0005) kupitia makubaliano ya Eneo Maalumu la Uwekezaji kwa Wanyamapori kwa wawekezaji wawili kwenye jumla ya maeneo 13, ingawa maeneo hayo hayakupata idhini ya waziri kuwa vitalu vya uwindaji kama inavyotakiwa kisheria. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Ripoti hiyo iliyowasilishwa bungeni jijini Dodoma jana Jumatatu na CAG Charles Kichere imesema hali hiyo inaonesha kuwa, menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania haikuzingatia majukumu ya Waziri wa Maliasili na Utalii kabla ya kutoa hati husika.
“Ni maoni yangu kuwa, kutoa hati hizo kwa maeneo ambayo hayajapata idhini ya waziri ni kukiuka kwa kiasi kikubwa Kanuni za Eneo Maalumu la Makubaliano ya Uwekezaji wa Wanyamapori za Mwaka 2020 na kuleta shaka kuhusu uwazi na uadilifu wa mchakato wa ugawaji wa maeneo hayo.
“Napendekeza Serikali ihakikishe TAWA inazuia ugawaji wa maeneo maalumu ya uwekezaji kwa wanyamapori bila idhini ya Waziri,” amesema.
Leave a comment