Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa TAMISEMI yatenga bil. 17.79 kwa ajili uchaguzi serikali za mitaa
Habari za Siasa

TAMISEMI yatenga bil. 17.79 kwa ajili uchaguzi serikali za mitaa

Spread the love

WIZARA Ofisi ya Rais-TAMISEMI, imetenga fedha kiasi cha Sh. 17.79 bilioni, kwa ajili ya uratibu na kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 16 Aprili 2024 na Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa, akiwasilisha bungeni jijini Dodoma, makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha ujao wa 2024/25.

“Katika mwaka wa 2024/25 TAMISEMI imetenga Sh. 17.79  bilioni kwa ajili ya kuratibu na kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024. Kati ya fedha hizo Sh. 8.00 bilioni ni fedha kutoka serikali kuu kwa ajili ya uratibu Ofisi ya Rais – TAMISEMI (Makao Makuu) na Sh.  9.79 bilioni ni mchango wa halmashauri kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya kugharamia uchaguzi huo,” amesema Mchengerwa.

Amesema mbali kiasi hicho cha fedha kilichotengwa na TAMISEMI kwa ajili ya uchaguzi huo, katika mwaka wa fedha wa 2023/24, ilitenga Sh. 12.00 bilioni kwa ajili ya maandalizi yake, ambapo hadi Machi 2024, ilipokea Sh. 5.6 bilioni huku zilizosalia zikihusisha shughuli za ununuzi ambazo taratibu zake zinaendelea.

Katika hatua nyingine, Mchengerwa aliliomba Bunge liidhinishe bajeti nzima ya TAMISEMI kwa 2024/25  kiasi cha Sh. 10.12 trilioni, ambapo Sh. 6.70 trilioni ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida ikiwemo mishahara ya watumishi na Sh. 3.41 trilioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!