Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge laagiza uchunguzi ‘Super Market’
Habari za SiasaTangulizi

Bunge laagiza uchunguzi ‘Super Market’

Spread the love

 

BUNGE la Tanzania, limeiagiza Serikali ifanye uchunguzi katika maduka makubwa ‘Super Market’, ili kuondoa biadhaa za kughushi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Agizo hilo limetolewa leo Jumatano, tarehe 16 Juni 2021 na Mwenyekiti wa Bunge, Azzan Zungu, baada ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe, kusema Serikali iko mbioni kutunga sheria ya kulinda haki na maslahi ya watumiaji nchini.

Mwenyekiti huyo wa Bunge, amedai kwamba, hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la bidhaa za kughushi ‘feki’, katika maduka hayo, hali inayoathiri wanunuzi wake.

“Waziri hebu tumeni watu wenu kwenye Ma-Super Market makubwa, muone dettol (dawa ya kuwa wadudu) na sabuni za kuogea zote feki. Watu wanalipa pesa nyingi, wanatumia vitu sio halali na pesa wanazolipa,” amesema Zungu na kuongeza:

Mussa Zungu

“Chunguzeni Super Market zote mkatizame, dettol ya zamani ukiitia maji inakuwa nyeupe, leo ukiitia maji inakuwa nyeusi. Pamoja na sabuni ambazo zimeandikwa majina, makubwa lakini feki.”

Awali, Kigahe alisema Serikali itatunga sheria hiyo, akimjibu Mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Oscar Kikoyo, aliyehoji lini Serikali itaunda mamlaka yenye nguvu ya kulinda haki na maslahi ya watumiaji.

“Mihimili muhimu ya uchumi wa soko ni mamlaka za udhibiti, Tume ya Ushindani (FCC) na mamlaka ya kulinda haki na maslahi ya watumiaji (final consumer). Je, ni lini Serikali itaunda mamlaka yenye nguvu ya kulinda haki na maslahi ya watumiaji nchini?” Alisema Kikoyo na kuongeza:

“Je, Serikali ina mpango gani wa kutunga Sheria ya Kuwalinda watumiaji?”

Katika majibu yake kuhusu maswali hayo, Kigahe alisema “ili kumlinda mlaji tunataka tuwe na sheria ya moja kwa moja, itakayohakikisha inasimamia na kumlinda mlaji.”

Waziri Mkuu akihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Kigahe alisema katika mwaka wa fedha ujao wa 2021/22, itaanzisha rasmi Baraza la Kumtetea na Kumlinda Mlaji (NCAC), ambalo litakuwa na jukumu la kisheria kusiammia haki za mlaji.

“ Serikali imekamilisha uundaji wa NCAC, ambalo litakuwa na jukumu la kisheria kusimamia haki za mlaji. Katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kukamilisha taratibu zauanzishwaji wa Baraza hilo,” alisema Kigahe.

2 Comments

  • Asante ndugu zungu sio madawA and sabuni ndio feki hata vya kula vingi ndani vinauzwa vimepita muda wake wa kuliwa vyombo vya matumizi ya nyumba vingi ni feki kwa kweli super market kaa lamoto kwa kuwa idadi ya watumiaji hatuellewi nini maana ya super market sasa ndio sababu ya kubambikiwa bidha na zilizo pita muda wake ktk super market zetu unauziwa mkate haauna ya mwanzo wala ya mwisho kweli haki io

  • Siyo elimu. Tumekuwa wajinga, hatutumii elimu zetu.
    Pia, hii ni kazi ya Tanzania Bureau of Standards na Tanzania Food Authority (?) Hawafuatilii wanachoruhusu.
    Wawe na maeneoya kupokea malalamiko.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!