WATU 80 wameuawa na wengine zaidi ya mia tatu kujeruhiwa, baada ya bomu lililotegwa kwenye gari kulipuka jirani na ubalozi wa Ujerumani mjini Kabul, Afghanistan, anaandika Mwandishi wetu.
Maafisa nchini humo wanasema mlipuko mkubwa ambao umetokea katika eneo la makazi ya wanadiplomasia mapema asubuhi.
https://youtu.be/MVTHqb8zbSQ
Wingu la moshi mkubwa lilikuwa limetanda na kuonekana katika maeneo mengi ya mji wa Kabul.
Aidha nyumba zilizokuwa jirani na bomu hilo lilipolipuka pia zilipatwa na madhara kwa madirisha na milango kupasuka.
Mwezi uliopita wapiganaji wa Taliban walitangaza kuanza kufanya mashambulizi na kusema kuwa yatakuwa yanalenga majeshi ya kigeni.
Leave a comment