Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea amtoa jasho Mwijage bungeni
Habari za Siasa

Kubenea amtoa jasho Mwijage bungeni

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo. Picha ndogo Charles Mwijage Waziri wa Viwanda
Spread the love

WAZIRI wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage alijikuta katika wakati mgumu baada ya kushindwa kujibu swali la nyongeza la Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema), anaandika Dany Tibason.

Mwijage alijikuta akipiga siasa na kutoa majibu yaliyoelezwa kuwa ni ya uchochezi kwa wapiga kura wa jimbo la Ubungo badala ya kushindwa kutoa majibu sahihi kama alivyouliza muuliza swali la nyongeza ambaye ni Kubenea.

Katika swali la nyongeza Kubenea alitaka serikali ieleze ni lini itaweza kutatua migogoro ambayo inajitokeza katika viwanda ambavyo vipo Ubungo kutokana na wafanyakazi kutolipwa mishahara yao kwa wakati.

Kubenea mesema uwekezaji hauendani na matakwa yanayotakiwa na kuuliza ni lini serikali itaweza kutatia migogoro mikubwa kati ya wawekezaji wa kiwanda cha Urafiki kutokana na kuwepo kwa malalamiko kwa wafanyakazi kutolipwa mishahara kwa wakati.

Awali katika swali la msingi la mbunge wa Viti Maalum, Mwanne Mchemba (CCM) alitaka kujua ni lini serikali italeta wawekezaji katika mkoa wa Tabora.

“Mkoa wa Tabora upo tayari kwa ajili ya uwekezaji wa EPZ uliotengewa eneo katika wilaya ya Uyui, Je ni lini serikali italeta wawekezaji katika mkoa wa Tabora?” alihoji.

Akijibu swali la nyongeza la Kubenea, Charles Mwijage, amesema viwanda vilivyopo Ubungo vinaweza kuajili vijana zaidi ya 400.

“Kama viwanda vilivyopo ubungo nilitamani kuviamishia katika jimbo langu kwani viwanda hivyo ni mtaji mkubwa kwa wapiga kura wa Ubungo hivyo viwanda hivyo vinaweza kuajiri vijana zaidi ya 400”  amesema Mwijage.

Amesema mchakato wa kutenga eneo mkoa wa Tabora kwa ajili ya EPZ ulianza mwaka 2010 baada ya wizara kuelekeza uongozi wa mkoa kutenga eneo lisilopungua ukubwa wa hekari 2,000.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!