Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani
Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the love

MADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya elimu ya usalama barabarani yalivyo wafumbua macho na kuwafanya kufahamu sheria mbalimbali za barabarani na hivyo kuendelea na kazi yao wakiwa salama. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Wamesema hayo mbele ya waandishi wa habari waliokuwa wametembelea kijiwe cha bodaboda cha Kijiwe Pesa ambapo baadhi ya bodaboda walikuwa wakifanya tathmini kuhusu mafunzo waliyopata kutoka Amend kwa ufadhili wa Ubalozi wa Uswisi ambao wameendelea kufanikisha kutolewa kwa mafunzo hayo.

Madereva hao bodaboda katika kijiwe hicho wamesema awali hawakuwa wakifahamu vema sheria za usalama barabarani hasa taa zinazoongoza magari na jinsi ya kupita kwenye makutano ya barabara ilikuwa ni kitendawili kwao.

“Kupitia mafunzo ya usalama barabarani ambayo tumeyapata kutoka kwa wenzetu wa Amend kwa kushirikiana na wadau wengine kama Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama barabarani sasa tunafahamu vema sheria za usalama barabarani pamoja na alama zilizopo,” amesema dereva bodaboda Jonathan Chidawi

Kwa upande wake Amiri Matimba ambaye ni  Msaidizi wa Miradi kutoka Shirika la Amend Tanzania anasema wamefanikiwa kutoa mafunzo kwa madereva bodaboda 47 kwa wiki ya kwanza jijini Dodoma.

Ameongeza kuwa  wanaendelea kutembea katika vijiwe mbalimbali vya bodaboda kwa ajili ya kuhamasisha maofisa hao kusafirishaji(bodaboda)kujiunga katika mafunzo hayo yanayotolewa bila gharama yoyote.

Wakati huo huo Mkufunzi wa Mafunzo hayo ambae pia ni Katibu wa Chama cha Walimu wa madereva Tanzania (CHAWATA) Massava Ponera akieleza tathimi ya mafunzo hayo toka walipoanza hadi walipofikia amesema mafunzo yanaendelea na madereva wengi wamefikiwa na mafunzo hayo.

Amefafanua kwa Dodoma hiyo ni awamu ya pili kutolewa kwa mafunzo hayo ambayo yamedhaminiwa na ubalozi wa Uswisi ili kuwezesha elimu ya usalama barabarani inafika kwa kundi la bodaboda ambalo jamii siku zote hulitazama kwa jicho la tofauti na kuamini ni wavunjaji wa sheria wakubwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!