Hivyo alimuagiza Waziri huyo wa Kilimo kuhakikisha anaweka mameneja kwenye kila skimu za umwagiliaji mkoa ili waweze kutoa huduma za karibu na kuepusha migogoro ikiwemo ya mipaka kwa wakulima na wafugaji.
Mmoja wa wakazi wa kijiji hicho Mercy Maneno alisema licha ya kuwa na ardhi nzuri na ya rutuba lakini bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mazao kulingana na kilimo kutokana na kukosa mabwawa makubwa ua kuhifadhi maji kwa ajili ya kilimo Cha umwagiliaji.
Naye Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Sophia Mjema aliwataka wananchi, wanachama na wapenzi wa CCM kuendelea kutangaza sera na Ilani ya CCM kwa kutangaza mazuri yote aliyofanya Rais Samia Suluhu Hassan.
Alisema kwa Sasa Tanzania Kuna shule Nzuri ambazo wanafunzi wengi hupata elimu bure kuanzia darasa la sifuri Hadi kidato Cha sita Mambo ambayo alisema kuwa yote ni mipango na utekekezaji Ilani ya Chama.
Hivyo aliishauri jamii na wanachama wa CCM na wasio wa CCM kukaa tayari kusubiri mafunzo ya sera na itukadi ya CCM yatakayotokewa hivi karibuni.
Leave a comment