Akiongea wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kwenye mgodi wa Barrick North Mara, Dk.Ngido alisema Barrick inayo programu maalumu ya kuwapa wanawake kipaumbele katika suala la ajira , kuwajengea uwezo wa shughuli za uchimbaji madini na kuwajengea mazingira bora zaidi ya kazi.
“Msijisikie kuwa second class (daraja la pili), onesha kuwa mnaweza na naamini uwezo mnao,” alisema Ngido katika maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa na Wafanyakazi Wanawake kutoka mgodi huo.
Kwa upande wake,Meneja Mkuu wa mgodi huo, Apolinary Lyambiko, alisema anafurahishwa kuona idadi ya wafanyakazi wanawake katika mgodi huo imeongezeka uliganisha na miaka ya nyuma, na amewamiminia sifa kwamba wengi wao wanaonesha bidii na ufanisi mkubwa katika utekelezaji wa majukumu yao kazini.
“Takwimu za mwaka jana na sasa zinaonesha kuna ongezeko la wafanyakazi wanawake katika mgodi wetu, na wengi wao wanafanya kazi nzuri. Hivyo tutaendelea kuwapa fursa, siyo tu kujishughulisha na uchimbaji, bali na kuwamotisha pia,” amesisitiza Lyambiko na kuwataka kuendelea kuonesha uwezo mkubwa kazini na kujenga tabia ya kujiamini.
Lyambiko, alisema pia mgodi utaendelea kutekeleza sera yake ya kupinga vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa kuhakikisha vitendo hivyo vinakuwa katika kiwango cha sifuri katika mgodi huo.
Leave a comment