Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Dodoma acharuka waumini kuimba, kukata mauno
Habari Mchanganyiko

Askofu Dodoma acharuka waumini kuimba, kukata mauno

Spread the love

KANISA la Maombi na Maombezi kwa Mataifa yote (RUTACH) limepiga marufuku waumini wake kuacha mara moja kukata mauno pindi wanapokuwa wakiimba kwaya au katika kipindi cha sifa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea)

Katazo hilo limetolewa leo tarehe 20 Februari, 2022 na Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Living Mwambapa alipokuwa akihubiri katika ibada maalumu ya nguvu ya kulikomboa taifa na kuwahimalisha viongozi wa ngazi zote.

Mwambapa amesema kanisa siyo sehemu ya kufanya mambo yanayoshabihiana na yale ya kishetani badala yake pawe sehemu ya kutafuta Mungu aliye hai.

“Natangangaza kwa makanisa yote kuachana na tabia ya kufanya huduma ya uimbaji kwa kukata mauno au kuvaa nguo ambazo hazina staha.

“Hatuwezi kuruhusu mitindo ya kishetani kuingia makanisani, kuvaa nguo ambazo hazina staha au kukata mauno wanapokuwa kwenye huduma kanisani kwa kufanya hivyo ni kuibua hisia za kuwaondoa katika uwepo wa Kimungu,” amesema.

Amesema haiwezekani kufanya kanisa kama sehemu ya kitega uchumi kwa kufanya mambo ambayo yanayofanywa na watu wa mataifa.

” Kanisa ni sehemu takatifu ya kumlilia Mungu kwa kuishi katika matendo ya kumpendeza Mungu,hatuwezi kuruhusu mavazi ya ovyo au kukata mauno wakati wa uimbaji.

“Makanisani kuna watu nao wana mwili na Roho, hivyo siyo jambo zuri kuingizana kwenye majaribu kwa kukata mauno au kuvaa nguo ambazo hazina utukufu” ameeleza Askofu Mwambapa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

error: Content is protected !!