Friday , 10 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwinyi aungana na Samia kuuaga mwili wa baba yake
Habari za Siasa

Dk. Mwinyi aungana na Samia kuuaga mwili wa baba yake

Spread the love

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amejumuika na wananchi, viongozi mbalimbali wa Kitaifa akiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Rais Mstaafu wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mzee Ali Hassan Mwinyi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Shughuli za kuaga mwili wa Mzee Mwinyi zimefanyika katika Uwanja  wa Amaan, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja leo tarehe 2 Machi 2024.

Pia Rais Samia ameongoza viongozi mbalimbali kutoa salamu za rambirambi  na pole kwa watanzania na familia ya Marehemu Mzee Ali Hassan Mwinyi pamoja na kutoa heshima za mwisho kwa Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi katika uwanja huo.

Viongozi mbalimbali wameshiriki wakiwemo wa Serikali ya  SMT na SMZ,  wa Vyama vya siasa, Vyombo vya ulinzi na usalama, Dini, Waheshimiwa Mabalozi pia wawakilishi wa nje ya Tanzania wakiwemo  Namibia, Burundi na Comoro walitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Nchi zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina awavaa mawaziri wanaompelekea majungu Rais Samia

Spread the loveMBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amewataka baadhi ya mawaziri...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

error: Content is protected !!