Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amejumuika na wananchi, viongozi mbalimbali wa Kitaifa akiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Rais Mstaafu wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Shughuli za kuaga mwili wa Mzee Mwinyi zimefanyika katika Uwanja wa Amaan, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja leo tarehe 2 Machi 2024.
Pia Rais Samia ameongoza viongozi mbalimbali kutoa salamu za rambirambi na pole kwa watanzania na familia ya Marehemu Mzee Ali Hassan Mwinyi pamoja na kutoa heshima za mwisho kwa Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi katika uwanja huo.
Viongozi mbalimbali wameshiriki wakiwemo wa Serikali ya SMT na SMZ, wa Vyama vya siasa, Vyombo vya ulinzi na usalama, Dini, Waheshimiwa Mabalozi pia wawakilishi wa nje ya Tanzania wakiwemo Namibia, Burundi na Comoro walitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Nchi zao.
Leave a comment