Saturday , 11 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hamahama Ngorongoro kutikisa maandamano ya Chadema Arusha
Habari za Siasa

Hamahama Ngorongoro kutikisa maandamano ya Chadema Arusha

Spread the love

MAELFU ya wanachama na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wanatarajia kushiriki maandamano ya amani yaliyoandaliwa na chama hicho, kudai katiba mpya na kupinga ugumu wa maisha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Hayo yamebainishwa leo tarehe 26 Februari 2024 na Makamu Mwenyekiti wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalim, akielezea maandalizi ya maandamano hayo yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumanne, jijini Arusha, ambapo amesema yamefikia asilimia 97.

Mwalim amesema watu 1,000 jamii ya kimasai ni miongoni mwa washiriki wa maandamano hayo, ambao watayatumia kupaza sauti zao kupinga zoezi la Serikali kuwahamisha katika hifadhi ya Ngorongoro.

Mbali na wamasai, Mwalim amesema watu 1,800 kutoka mkoa wa Kilimanjaro na 2,300 kutoka Manyara, ni miongoni mwa waliojisairi kushiriki maandamano hayo ya hiari.

“Jamii ya wamasai zaidi ya 1,000 ambao watatoka eneo la Ngorongoro, Simanjiro na Tanga walikopelekwa ambao wamejiandikisha kushiriki maandamano hayo. Wengine ni jamii kubwa ya wafanyabiashara ndogo na wa kati Arusha,” amesema Mwalim na kuongeza:

“Mafuriko hayo yataonyesha haja na kiu ya matumaini ya watanzania wanayotaka. Yatabeba kielelezo halisi cha ugumu wa maisha, madai ya katiba mpya na miswada mitatu ambayo imepitishwa bungeni.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina awavaa mawaziri wanaompelekea majungu Rais Samia

Spread the loveMBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amewataka baadhi ya mawaziri...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

error: Content is protected !!