Saturday , 11 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO
Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Rais wa Urusi, Vladimir Putin
Spread the love

SERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake, ili kujihami na vitisho vya kiusalama, kufuatia kupanuka kwa Jumuiya ya Kujihami ya Nchi za Magharibi (NATO). Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Wizara ya Ulinzi ya taifa hilo, imesema Rais wa Urusi, Vladimir Putin, ametia saini amri ya kuongeza idadi ya wanajeshi 170,000 ili kufikia 1,320,000, sawa na ongezeko la asilimia 15.

Mtandao wa BBC Swahili umeripoti kuwa, uamuzi huo unatokana na ongezeko la nchi jirani za Urusi, kujiunga na NATO, ikiwemo Finland iliyojiunga hivi karibuni, baada ya Urusi kuanzisha operesheni ya kijeshi nchini Ukraine, ikipinga uamuzi wake wa kuomba kujiunga na jumuiya hiyo.

Katika taarifa yake, Wizara ya Ulinzi Urusi imedai taifa hilo linakumbwa na vitisho vya kiusalama, kutokana na ongezeko la vikosi vya kijeshi vya NATO, karibu na mpaka wake.

Urusi imekuwa ikipinga majirani zake kujiunga na NATO kwa madai kuwa hatua hiyo inahatarisha usalama wake kwa kuwa ni sawa na kukaribisha miundombinu ya kijeshi ya jumuiya nchini humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

error: Content is protected !!