Thursday , 9 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Balozi Dk. Slaa naye adaiwa kukamatwa
Habari za SiasaTangulizi

Balozi Dk. Slaa naye adaiwa kukamatwa

Spread the love

BALOZI na Mwanasiasa maarufu nchini, Dk. Wilbroad Slaa anadaiwa kukamatwa na Jeshi la Polisi nyumbani kwake Mbweni jijiji Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali, akiwamo Askofu Emmaus Mwamakula zinasema, Dk. Slaa amekatwa leo Jumapili mchana ikiwa ni siku moja baada ya kukamatwa kwa Wakili Boniface Mwambukusi na Mdude Nyagali.

Dk. Slaa ambaye pia aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Chadema, ni mmoja wa wanasiasa wanaopinga mkataba wa uwekezaji kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai.

 

Kukamatwa kwa Dk. Slaa pamoja Mwabukusi  kumekuja siku chache baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi kuutangazia ulimwengu, kwamba “kuna njama za kumuangusha Rais wa Jamhuri, Dk. Samia Suluhu Hassan.”

Akiandika kupitia mtandao wake wa kijamii, Askofu Mwamakula anasema,

“taarifa zilizotufikia hivi punde ni kuwa Balozi Dk . Wilbroad Slaa amekamatwa na Jeshi la Polisi nyumbani kwako jijini Dar es Salaam.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online kwa taarifa zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Madiwani Msalala wampa tano DED kwa kuongeza mapato

Spread the loveMKURUGENZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, mkoani Shinyanga, Khamis...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kimbunga Hidaya chaua 5, kaya 7,027 zikikosa makazi

Spread the loveSERIKALI imetoa tathmini ya athari za kimbunga Hidaya, kilichotokea tarehe...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yaainisha mpango wa kusaidia wachimbaji wadogo

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameainisha mpango wa Serikali wa...

Habari za SiasaTangulizi

Bashiru Ally aivaa serikali kukalia vibali vya wahadhiri

Spread the loveMBUNGE wa kuteuliwa, Dk. Bashiru Ally amesema vikwazo vinavyoendekezwa na...

error: Content is protected !!