Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu awataka vijana kufanya kazi, kuacha utegemezi
Habari Mchanganyiko

Askofu awataka vijana kufanya kazi, kuacha utegemezi

Spread the love

ASKOFU mkuu wa kanisa la The Potter’s House Tanzania (PHCT), Ruth Kusenah amewataka vijana  wote nchini kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kujiongezea kipato wao wenyewe na taifa kwa ujumla. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma… (endelea).

Ametoa rai hiyo leo tarehe 12 Machi 2023  katika ibada maalumu ya kutambulisha hati ya usajili wa kudumu wa kanisa hilo lenye makao yake makuu jijini Dodoma katika kata ya Ipagara mtaa wa Mlimwa west.

Amesema kuwa kanisa hilo pamoja na kuwa linawalea watu kiroho lakini bado linasisitiza waumini wake na jamii kwa ujumla kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kujipatia kipato pamoja na kulifanya taifa kuepukana na vijana wengi ambao ni tegemezi.

“Kwa sasa kanisa letu limepata usajili wa kudumu tunawashukuru sana viongozi wa serikali kwa kuweza kutambua umuhimu wa uhuru wa kuabudu, kanisa linaendelea kutoa huduma ya kiroho lakini pia tunasisitiza katika utendaji wa kazi kwa bidii kwa kazi ni mpango wa Ki-mungu pia.

“Mandiko Matakatifu yanaelekeza zaidi kuwa asiyefanya kazi na asile, lakini pia yanaelekeza kuwa Mungu atabariki kazi za mikono yetu na atabariki mashambani na mjini na aingiapo shambani na atokapo hivyo kufanya kazi ni mpango wa Mungu mwenyewe” amesisitiza Askofu Mkuu Ruthi.

Sambamba na hilo Askofu huyo amesema kanisa litashirikiana na serikali katika kufanya kazi ya kimaendeleo pamoja na kusikiliza mipango iliyo mema kwa taifa na watu wake.

Naye katibu mkuu wa kanisa hilo, Festo Lesirwa, amesema kanisa litafanya kazi na serikali kwa ukaribu ikiwa ni pamoja na kuishauri serikali, kuipongeza na kuionya pale inapokuwa imeenda kinyume lakini kwa kutumia lugha za staha.

Aidha, amesema kuwa kanisa litahakikisha linalinda amani ya nchi kwa kujenga misingi ya mshikamano upendo na umoja ili kila mmoja aweze kufanya kazi kwa amani na utulivu bila kuwepo kwa migongano ya aina yoyote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!