Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Michezo Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi
Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the love

MASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania ng’ombe yanazidi kutimua vumbi huku timu kadhaa zikiendelea kumenyana katika hatua ya makundi. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Katika mchenzo uliochezwa leo tarehe 1 Machi 2023, ulizikutanisha timu mahasimu wa jadi  za Kamongo na Darton zimeshindwa kupata mbabe baada ya kutoka suluhu ya kutofungana kwenye mchezo uliopepetwa katika Uwanja wa Bubu Kata ya Makurumla Manispaa ya Ubungo.

Katika mchezo huo uliokusanya mashabiki lukuki kwa kila timu, ambapo timu hizo zilishindw kupata mbabe katika dakika 90 za mchezo huo.

Mchezo huo ambao mwamuzi wa kati alikuwa Hamis Pondamali akisaidiwa na waamuzi wa pembeni ambao mara zote walikuwa na kibarua cha kufuatilia hatua zote muhimu katika mchezo huo.

Akizungumza mmoja wa mashabiki wa mpira wa miguu ambaye alihudhuria uwanjani hapo, Saidi Mjeshi amesema kwa muda wa zaidi ya miaka 10 timu za mpira wa miguu pamoja na mashabiki walikosa burudani ya soka na sasa wanaona mwanga mpya.

Diwani wa Kata ya Makurumla, Bakari Kimwanga (aliyesimama) akiwatambulisha wanahabari za michezo nchini Jimmy Chika ( kulia), Juma Kasesa (katikati) kwa Mjumbe wa Kamati ya Mashindano ya Kimwanga CUP, Issa Salumu ( kushoto).

“Huyu diwani (Bakari Kimwanga) amefanya jambo kubwa kwanza Serikali ya mama Samia inataka michezo na yeye ameileta kwa kweli sasa tuna uhalika wa kupata burudani kila siku jioni hapa Uwanjani kwetu kwa Bubu.

“Lakini tu kinachovutia ni zawadi iliyoandaliwa na diwani kwa mshindi wa kwanza ya ng’ombe na sasa tunashuhidia kila timu ikihangaika kujiweka sawa ili mradi ijikusanyie alama tatu muhimu katika kila mchenzo.” amesema Mjeshi

Akizungumza na waandishi wa habari uwanjani hapo, Diwani wa Kata ya Makurumla, Bakari Kimwanga ambaye ndiye aliandaa mashindano hayo, amesema kuwa amedhamiria kukuza vipa ji kupitia mpira wa miguu.

” Kwetu tunaendelea kutoa nafasi za taasisi mbalimbali ambazo zinataka kuja kudhamini mashindano yetu lengo likiwa ni kuwa na mashindano yaliyo bora na ya mfano.

“Kubwa tunashuhudia idadi kubwa ya mashabiki kila siku tunaona uwanja unakusanya zaidi ya watu 1500 hadi 2000 ambao wanakuja kupata burudani.


“Milango yetu ipo wazi kwa mtu au taasisi yoyote inayotaka kuja kudhamini mashindano haya ya Kimwanga CUP ikiwamo kuboresha zawadi kwa washindi.

“Tunataka kuonyesha burudani hasa kwa jamii yetu,” amesema Kimwanga

1 Comment

  • @THINK/Dedication/Remember”@ EMPLOY/US THEM ALL – ALL TANZANIAN HAS JOB TO DO

    In 2021, the unemployment rate in Tanzania remained nearly unchanged at around 32.74 percent. With a decline of 0.04 percentage points, there is no significant change to 2020. Over the observed period, the unemployment rate has been subject to fluctuation.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!