Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mambo matano kuteka mkutano wa faragha wa mawaziri Arusha
Habari za Siasa

Mambo matano kuteka mkutano wa faragha wa mawaziri Arusha

Spread the love

 

KATIBU Mkuu Kiongozi, Dk. Moses Kusikulika, amesema mada tano zitajadiliwa katika mkutano wa faragha wa siku tatu wa mawaziri na makatibu wa wizara, unaofanyika jijini Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endele).

Dk. Kusiluka ametaja mada hizo leo Alhamisi tarehe 2 Machi 2023, katika ufunguzi wa mkutano huo uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan, jijini Arusha.

Ametaja mada hizo kuwa ni, maelekezo ya Rais Samia kwa watendaji hao wa Serikali, taratibu za uendeshaji, mahusiano na mipaka ya utendaji kazi serikalini, utaratibu wa utoaji maamuzi makubwa ya kisera serikalini na usimamizi wa rasilimali watu na uhusiano wa Serikali na sekta binafsi.

Mbali na mada hizo kuu, Dk. Kusiluka amesema kutakuwa na mada ndogo 17, ambazo zitatolewa na watoa mada 17, akiwemo Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda; Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Balozi Ombeni Sefue na Mshauri wa Rais katika masuala ya majadiliano, Prof. Palamagamba Kabudi.

Wengine ni Leonard Msusa, kutoka sekta binafsi. Mtaalamu wa masuala ya rasilimali watu, Zuhura Muro na aliyekuwa Katibu Mkuu Utumishi, Dk, Laurian Ndumbaru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!