KATIBU Mkuu Kiongozi, Dk. Moses Kusikulika, amesema mada tano zitajadiliwa katika mkutano wa faragha wa siku tatu wa mawaziri na makatibu wa wizara, unaofanyika jijini Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endele).
Dk. Kusiluka ametaja mada hizo leo Alhamisi tarehe 2 Machi 2023, katika ufunguzi wa mkutano huo uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan, jijini Arusha.
Ametaja mada hizo kuwa ni, maelekezo ya Rais Samia kwa watendaji hao wa Serikali, taratibu za uendeshaji, mahusiano na mipaka ya utendaji kazi serikalini, utaratibu wa utoaji maamuzi makubwa ya kisera serikalini na usimamizi wa rasilimali watu na uhusiano wa Serikali na sekta binafsi.
Mbali na mada hizo kuu, Dk. Kusiluka amesema kutakuwa na mada ndogo 17, ambazo zitatolewa na watoa mada 17, akiwemo Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda; Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Balozi Ombeni Sefue na Mshauri wa Rais katika masuala ya majadiliano, Prof. Palamagamba Kabudi.
Wengine ni Leonard Msusa, kutoka sekta binafsi. Mtaalamu wa masuala ya rasilimali watu, Zuhura Muro na aliyekuwa Katibu Mkuu Utumishi, Dk, Laurian Ndumbaru.
Leave a comment