Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mambo matano kuteka mkutano wa faragha wa mawaziri Arusha
Habari za Siasa

Mambo matano kuteka mkutano wa faragha wa mawaziri Arusha

Spread the love

 

KATIBU Mkuu Kiongozi, Dk. Moses Kusikulika, amesema mada tano zitajadiliwa katika mkutano wa faragha wa siku tatu wa mawaziri na makatibu wa wizara, unaofanyika jijini Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endele).

Dk. Kusiluka ametaja mada hizo leo Alhamisi tarehe 2 Machi 2023, katika ufunguzi wa mkutano huo uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan, jijini Arusha.

Ametaja mada hizo kuwa ni, maelekezo ya Rais Samia kwa watendaji hao wa Serikali, taratibu za uendeshaji, mahusiano na mipaka ya utendaji kazi serikalini, utaratibu wa utoaji maamuzi makubwa ya kisera serikalini na usimamizi wa rasilimali watu na uhusiano wa Serikali na sekta binafsi.

Mbali na mada hizo kuu, Dk. Kusiluka amesema kutakuwa na mada ndogo 17, ambazo zitatolewa na watoa mada 17, akiwemo Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda; Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Balozi Ombeni Sefue na Mshauri wa Rais katika masuala ya majadiliano, Prof. Palamagamba Kabudi.

Wengine ni Leonard Msusa, kutoka sekta binafsi. Mtaalamu wa masuala ya rasilimali watu, Zuhura Muro na aliyekuwa Katibu Mkuu Utumishi, Dk, Laurian Ndumbaru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!