Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Hiki hapa alichokifanya Lema mara tu baada kuwasili Tanzania
Tangulizi

Hiki hapa alichokifanya Lema mara tu baada kuwasili Tanzania

Spread the love

 

MUDA mfupi baada ya kuwasili Tanzania akitokea uhamishoni nchini Canada, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema, amezindua matawi matatu ya chama hicho, yaliyoko mkoani Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Lema amezindua matawi hayo leo tarehe 1 Machi 2023, akiwa njiani kutokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), kuelekea mkoani Arusha kwa ajili ya kushiriki mkutano wa hadhara wa Chadema.

Matawi ya Chadema yaliyozinduliwa na Lema ni, Tawi la Njia Panda ya KIA, Tawi la King’ori na Siha, mkoani Kilimanjaro.

Baada ya kuzindua matawi hayo Lema aliwaaga wanachama wa Chadema walioshiriki tukio hilo kwamba analekea Arusha kwa ajili ya mkutano wa hadhara.

“Wapiganaji mimi hapa sikai, naomba kuzindua rasmi tawi hili kwa heshima ya wanachama wa Siha, ninakwenda kufanya mkutano wa hadhara,” amesema Lema.

Kwa sasa Lema ameshawasili mkoani Arusha, na yuko katika uwanja ulioandaliwa na Chadema kwa ajili ya mkutano huo. Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho, akiwemo mwenyekiti wake, Freeman Mbowe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!