RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewataka mawaziri kueleza mafanikio ya Serikali mara kwa mara, ili kudhibiti baadhi ya watu wanaofanya upotoshaji. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).
Akifungua mkutano wa faragha wa mawaziri na makatibu wakuu wa wizara, leo tarehe 2 Machi 2023, jijini Arusha, Rais Samia amesema viongozi wa umma wamekuwa wazito kusema mafanikio hayo na kuacha watu wengine kuendelea kufanya upotoshaji.
“Nataka kuwakumbusha umuhimu wa kuisemea serikali kama moja ya mawasiliano nje ya Serikali. Katika eneo hili hatujafanya vizuri sana, tumekuwa wazito kuyasemea mafanikio mengi tunayopata na hivyo kuacha watu wengine kuendelea kufanya upotoshaji. Kuna usemi unaosema uongo ukisemwa mara nyingi huwa ukweli,” amesema Rais Samia.
Mkuu huyo wa nchi amesema, kuna mwanasiasa mmoja jijini Arusha, aliwahi kudai kwamba serikali imetelekeza visima vya maji na kutumia fedha nyingi kupeleka maji kwa wananchi, huku akijua kwamba visima hivyo vilikuwa na maji ambayo hayakuwa salama kwa matumizi ya wananchi kwa kuwa yalikuwa na chumvi nyingi hivyo serikali ikaamua kuwapeleka maji baridi wananchi.
“Wizara inayohusika ilitakiwa kusimama haraka na kutoa ufafanuzi na kumueleza kwa nini visima viliachwa,” amesema Rais Samia.
Leave a comment