Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Slaa asema hana chama “nikialikwa CCM, ACT, CHADEMA nitakwenda”
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa asema hana chama “nikialikwa CCM, ACT, CHADEMA nitakwenda”

Balozi, Dk. Willbroad Slaa
Spread the love

 

BAADA ya kuibua mjadala kufuatia hatua yake ya kuhutubia mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), mkoani Arusha, Balozi Dk. Wilbroad Slaa, amesema hana chama. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Balozi Slaa ametoa kauli hiyo leo tarehe 28 Februari 2023, akihojiwa na Kituo cha Televisheni cha Azam, baada ya baadhi ya watu kudai kwamba yuko mbioni kurejea Chadema, alikojivua uanachama miaka minane iliyopita.

Mwanasiasa huyo ameeleza kuwa, yeye hana chama na kwamba hata vyama vingine vya siasa vikimualika kushiriki katika matukio yao yuko tayari kwenda.

“Kwa sasa sina chama, nikialikwa na Chadema nitakwenda na kuzungumza, nikialikwa na CCM pamoja na ACT Wazalendo nitakwenda pia na nitazungumza ,mimi ni Mtanzania ninayejua haki zangu za kisheria na kikatiba,” amesema Balozi Slaa.

Mjadala wa Balozi Slaa kurejea Chadema ulishika Kasi kufuatia ahadi yake ya kutaka kushirikiana na chama hicho katika kudai upatikanaji wa katiba mpya, pamoja nakukikosoa Chama Cha Mapinduzi (CCM), hadharani kwamba kimeshindwa kuongoza nchi.

Mbali na kushiriki mkutano huo wa Chadema uliofanyika Karatu, mkoani Arusha, katika siku za karibuni Balozi Slaa amekuwa akishiriki matukio mbalimbali yanayoandaliwa na Chadema, hususa mikutano ya kidigitali inayofanyika kupitia mitandao ya Club House na Twitter Space, ambapo amekuwa akichangia mada kuhusu masuala ya kisiasa na mchakato wa katiba mpya.

Kabla ya kuachana na siasa hai mwaka 2015, Balozi Slaa alikuwa Katibu Mkuu wa Chadema, ambapo aliamua kujivua uanachama wa chama hicho kufuatia hatua ya chama chake kumpokea Edward Lowassa aliyetokea CCM na kuwa mgombea wake urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!