CHAMA cha ACT-Wazalendo, kimesema ndoto yake kuu si kushika dola bali kuwakomboa wananchi kiuchumi na kijamii. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
Hayo yameelezwa leo tarehe 18 Februari 2023 na Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, katika uzinduzi wa ahadi ya chama hicho kwa Watanzania, jijini Dar es Salaam.
“Chama cha siasa ni zaidi ya kusanyiko la watu, chama cha siasa lazima kiwe na malengo, chama cha siasa ni zaidi ya kushika dola. Malengo ya chama makini ni kuukomboa umma, kufanyia kazi changamoto za umma. Nafasi za kimadaraka ni nyenzo tu ya kutekeleza malengo ya chama cha siasa,” amesema Shaibu.
Amesema kuwa, ili ACT-Wazalendo itekeleze malengo hayo kinapaswa kujipanga kazi ambayo kimeanza kuifanya tangu kuanzishwa kwake Mei 2014.
“Sio kazi ndogo, sisi tumekusudia ili tuweze kutekeleza wajibu huo ipasavyo lazima tujenge taasisi imara ambayo inakubalika katika jamii ya watanzania,” amesema Shaibu.
AJALI MBAYA YATOKEA MLIMA WA ACT MZALENDO JIJINI MBEYA