Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ole Sendeka alitaka Bunge liache kulalamika, lichukue maamuzi
Habari za Siasa

Ole Sendeka alitaka Bunge liache kulalamika, lichukue maamuzi

Spread the love

MBUNGE wa Simanjiro, Christopher Olesendeka, amelitaka Bunge liache kulalamika kwa maamuzi yake iliyokwisha fanya, badala yake litoe maazimio ya kuwachukulia hatua watu wanaoshindwa kufanyia kazi maazimio yake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ole Sendeka ametoa ushauri huo leo Jumatano, tarehe 8 Februari 2023, bungeni jijini Dodoma, akichangia hoja zilizowasilishwa na kamati za kudumu za mhimili huo.

Ametoa kauli hiyo wakati akinukuu maneno ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, aliyoandika katika kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania, yaliyosema viongozi kukubali kufanywa vikaragosi ni dalili ya woga na si dalili ya heshima.

Ole Sendekea aliendelea kunukuu maneno ya Mwalimu Nyerere akisema, mwaasisi huyo wa Tanzania aliandika kuogopwa ni sifa na ada ya madikteta , viongozi halisi hawapendi kuishiriki na kwamba kujenga mazoea ya kutii viongozi hata katika mambo haramu ni dalili ya uoga na kukaribisha udikteta.

“Nayatumia maneno haya sababu sifurahii kuona Bunge likilalamika juu ya maamuzi ambayo mmekwisha fanya, ningependa tutoke na maazimio kwamba wale walioagizwa wayafanye tuwajue ni kina nani, wanapaswa kusimamia katika sekta hizo na Bunge lielezwe nani hawa wanaokaidi,” amesema Ole Sendeka na kuongeza:

“Sisi tuko hapa kwa niaba ya wananchi, tuchukue hatua kama hatuna mamlaka ya kuchukua hatua dhidi ya waziri mmoja mmoja, dhidi ya mtendaji mmoja mmoja, tuchukue hatua hata kwa wale ambao tuna mamlaka nao ili wawasimamie hawa ambao wamepewa dhamana.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

error: Content is protected !!