Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Idadi watu China yapungua kwa mara ya kwanza tangu 1961
Kimataifa

Idadi watu China yapungua kwa mara ya kwanza tangu 1961

Spread the love

 

IDADI ya watu nchini China imepungua kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 60, huku kiwango cha uzazi nchini humo kikifikia rekodi ya chini – watoto 6.77 kwa kila wanawake 1,000. Vimeripoti vyombo vya habari vya kimataifa … (endelea)

Idadi ya watu mnamo mwaka 2022 ilikuwa bilioni 1.4118 na imepungua kwa 850,000 kutoka mwaka 2021.

Kiwango cha watoto wanaozaliwa nchini China kimekuwa kikipungua kwa miaka, na hivyo kusababisha sera nyingi kupunguza muelekeo huo.

Lakini miaka saba baada ya kutupilia mbali sera ya mtoto mmoja, imeingia kile afisa mmoja alichoeleza kuwa “zama za ongezeko hasi la idadi ya watu”.

Kiwango cha watoto kuzaliwa mnamo mwaka 2022 pia kilipungua kutoka 7.52 mnamo 2021, kwa mujibu wa Ofisi ya Kitaifa ya Takwimu ya China, ambayo ilitoa takwimu hizo Jumanne.

Vifo pia vilizidi idadi ya waliozaliwa kwa mara ya kwanza mwaka jana – China iliingia katika kiwango cha juu zaidi cha vifo tangu mwaka 1976 – vifo 7.37 kwa kila watu 1,000, kutoka 7.18 mwaka uliopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!