Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Idadi watu China yapungua kwa mara ya kwanza tangu 1961
Kimataifa

Idadi watu China yapungua kwa mara ya kwanza tangu 1961

Spread the love

 

IDADI ya watu nchini China imepungua kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 60, huku kiwango cha uzazi nchini humo kikifikia rekodi ya chini – watoto 6.77 kwa kila wanawake 1,000. Vimeripoti vyombo vya habari vya kimataifa … (endelea)

Idadi ya watu mnamo mwaka 2022 ilikuwa bilioni 1.4118 na imepungua kwa 850,000 kutoka mwaka 2021.

Kiwango cha watoto wanaozaliwa nchini China kimekuwa kikipungua kwa miaka, na hivyo kusababisha sera nyingi kupunguza muelekeo huo.

Lakini miaka saba baada ya kutupilia mbali sera ya mtoto mmoja, imeingia kile afisa mmoja alichoeleza kuwa “zama za ongezeko hasi la idadi ya watu”.

Kiwango cha watoto kuzaliwa mnamo mwaka 2022 pia kilipungua kutoka 7.52 mnamo 2021, kwa mujibu wa Ofisi ya Kitaifa ya Takwimu ya China, ambayo ilitoa takwimu hizo Jumanne.

Vifo pia vilizidi idadi ya waliozaliwa kwa mara ya kwanza mwaka jana – China iliingia katika kiwango cha juu zaidi cha vifo tangu mwaka 1976 – vifo 7.37 kwa kila watu 1,000, kutoka 7.18 mwaka uliopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!