Thursday , 9 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Afungwa miaka 30 jela kwa kumbaka dada’ke
Habari Mchanganyiko

Afungwa miaka 30 jela kwa kumbaka dada’ke

Spread the love

 

MKULIMA Frank Kigomba, amehukumiwa na Mahakama ya Wilaya ya Kilolo,mkoani Iringa, kifungo cha miaka 30 jela pamoja na kulipa fidia ya Sh. 500,000, kwa kosa la kumbaka dada yake wa kuzaliwa ili apate utajiri. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi leo Jumamosi, kupitia ukurasa wake wa Twitter, Kigomba amepewa adhabu hiyo tarehe 5 Januari 2023 na hakimu wa mahakama hiyo, Tumaini Maleko.

“Mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakamani kwa kosa hilo ambapo alisomewa shtaka la kumbaka dada yake wa kuzaliwa tarehe 2 Januari 2023 ndani ya nyumba anayojenga kutokana na imani za kishirikina za kutaka kuwa tajiri baada ya kudanganywa na mganga kuwa akifanya hivyo atakuwa tajiri,” imesema taarifa ya Jeshi la Polisi na kuongeza:

“Baada ya mtuhumiwa kusomewa shtaka lake mahakamani hapo alikiri kosa na hivyo kupewa adhabu ya kifungo cha miaka 30 jela sambamba na kumlipa dada yake fidia ya kiasi hicho cha fedha Sh. 500,000.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yapunguza kodi ya makampuni kwa 20%

Spread the loveSERIKALI imepunguza kodi ya makampuni kwa asilimia 20, kutoka asilimia...

Habari Mchanganyiko

Mradi uliotaka kumng’oa madarakani Dk. Mpango waanza majaribio

Spread the loveMRADI wa maji wa Mwanga-Same-Korogwe, ambao Makamu wa Rais, Dk....

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Madiwani Msalala wampa tano DED kwa kuongeza mapato

Spread the loveMKURUGENZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, mkoani Shinyanga, Khamis...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kimbunga Hidaya chaua 5, kaya 7,027 zikikosa makazi

Spread the loveSERIKALI imetoa tathmini ya athari za kimbunga Hidaya, kilichotokea tarehe...

error: Content is protected !!