Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yafufua mradi wa maji uliotelekezwa miaka 60 iliyopita
Habari Mchanganyiko

Serikali yafufua mradi wa maji uliotelekezwa miaka 60 iliyopita

Spread the love

ZAIDI ya wananchi elfu tano wa Kijiji cha Msimba wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wanatarajiwa kunufaika na huduma ya maji safi na salama baada ya serikali kutumia  shilingi milioni 400  kukamilisha kuufufua mradi  wa maji uliotelekezwa na wajerumani miaka zaidi ya 60 iliyopita. Anaripoti Christina Haule, Kilosa … (endelea).  

Akitoa taarifa ya mradi huo,mkurugenzi wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira MORUWASA  Mhandisi Tamimu Katakweba alisema awali wananchi hao walikuwa wakitumia hayo jana mbele ya Waziri wa maji  Jumaa Aweso alipotembelea na kuzindua mradi huo.

Katakweba alisema wakazi hao walilazimika kutumia maji ya visima na mito kutokana na kukosa huduma ya uhakika ya maji safi na salama.

Alisema juhudi za kusogeza maji kwa wananchi ni safari ya kufikia malengo ya asilimia 85 ya upatikanaji wa maji Vijijini ikizidi kushika kasi na kutatua changamoto ya maji kwa wananchi.

 

Mkurugenzi wa MORUWASA alisema hiyo ni hatua nzuri ya mafanikio kama wataalamu kwa kuona sasa wananchi wanaaza kunufaika na miradi ya maji ukiwemo mradi huo utakaohudumia wakazi wa vijiji mbalimbali ikiwemo vya Mikumi na Msimba.

Naye Waziri wa maji Jumaa Aweso aliwaagiza wananchi wa vijiji hivyo kutunza vyanzo na miundombinu ya  miradi ya maji  uliotelekezwa  hapa na serikali ya kikoloni miaka zaidi ya sitini iliyopita ambapo sasa serikali imeufufua kwa lengo la kuendeleza dhamira ya kumtua mama ndoo kichwani.

Nao wananchi wa kijiji cha Msimba waliishukuru Serikali kwa jitihada zake za kuhakikisha wanapata maji safi waliyoyakosa kwa miaka mingi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!