MKULIMA Frank Kigomba, amehukumiwa na Mahakama ya Wilaya ya Kilolo,mkoani Iringa, kifungo cha miaka 30 jela pamoja na kulipa fidia ya Sh. 500,000, kwa kosa la kumbaka dada yake wa kuzaliwa ili apate utajiri. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi leo Jumamosi, kupitia ukurasa wake wa Twitter, Kigomba amepewa adhabu hiyo tarehe 5 Januari 2023 na hakimu wa mahakama hiyo, Tumaini Maleko.
“Mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakamani kwa kosa hilo ambapo alisomewa shtaka la kumbaka dada yake wa kuzaliwa tarehe 2 Januari 2023 ndani ya nyumba anayojenga kutokana na imani za kishirikina za kutaka kuwa tajiri baada ya kudanganywa na mganga kuwa akifanya hivyo atakuwa tajiri,” imesema taarifa ya Jeshi la Polisi na kuongeza:
“Baada ya mtuhumiwa kusomewa shtaka lake mahakamani hapo alikiri kosa na hivyo kupewa adhabu ya kifungo cha miaka 30 jela sambamba na kumlipa dada yake fidia ya kiasi hicho cha fedha Sh. 500,000.”
Leave a comment