Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani yapata Spika baada ya kura kurudiwa mara 15 kwa siku 4
Kimataifa

Marekani yapata Spika baada ya kura kurudiwa mara 15 kwa siku 4

Kevin McCarthy
Spread the love

 

KEVIN McCarthy amechaguliwa kuwa Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani huku kukiwa na majibizano makali ambayo karibu yashuhudiwe wawakilishi wa chama chake cha Republican washikane mashati. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

McCarthy hatimaye ameshinda nafasi hiyo baada ya duru 15 za upigaji kura, licha ya chama chake kuwa na kura nyingi katika bunge.

Ushindi wake umekuja baada ya kampeni kali ya shinikizo iliyofanywa na kushuhudiwa mubashara huku mmmoja wa waasi wa chama Matt Gaetz aliyekuwa hamuungi mkono mwanasiasa huyo alihimizwa kumpigia kura McCarthy. Congressman wa Florida alikuwa miongoni mwa watu sita ambao walijiuzulu Ijumaa.

Hapo awali, huku kukiwa na majibizano makali, Gaetz alikuwa karibu apigwe na Mwakilishi Mike Rogers – mfuasi wa McCarthy. Mbunge huyo wa Alabama alilazimika kuzuiwa na wenzake alipokuwa akimfokea na kumnyooshea kidole Bw Gaetz.

Nchini Marekani Spika wa bunge hilo huweka ajenda za Bunge na husimamia shughuli za kutunga sheria. Nafasi hiyo ni ya pili kwa ukubwa nchini Marekani kama ilivyo kwa makamu wa rais baada ya Rais wa Marekani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!