Friday , 10 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtendaji atumbuliwa akituhumiwa kufanya mapenzi ofisini, kuhonga fedha za Serikali
Habari Mchanganyiko

Mtendaji atumbuliwa akituhumiwa kufanya mapenzi ofisini, kuhonga fedha za Serikali

Mtendaji wa Kijiji cha Mbigili wilayani Kilosa, Briton Mshani
Spread the love

 

MTENDAJI wa Kijiji cha Mbigili wilayani Kilosa, Briton Mshani, amefukuzwa kazi kwa tuhuma za kufanya mapenzi ofisini, pamoja na kumhonga mpenzi wake kiasi cha Sh. 1 milioni, ambazo ni fedha zilizokuwa katika akaunti ya Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).

Akizungumza katika mkutano na wananchi wa Kilosa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Fatma Mwasa, amesema kwamba Mshani amefukuzwa kazi baada ya baadhi ya wananchi wa kijiji hicho kumtuhumu kwa rushwa na kufanya mapenzi ofisini.

“Mtendaji wa kijiji aliyoiba fedha halafu akamhonga nyumba ndogo akageuza ofisi ya kijiji kuwa gesti, ametoa hela kwa kuhamisha akaunti ya Serikali kwenda kwenye akaunti binafsi ya mwanamke wake, huyu ameshafukuzwa kazi,” amesema Mwasa.

Katika hatua nyingine, Mwasa ameagiza mtendaji huyo wa kijiji achukuliwe hatua za kisheria huku akiagiza mtu mwingine atafutwe kwa ajili ya kujaza nafasi yake.

Mbali na tuhuma hizo, Mshani alituhumiwa kuchukua fedha za wanakijiji kiasi cha Sh. 500,000 kwa ajili ya kuwasaidia kutatua mgogoro wa ardhi, hata hivyo alikanusha madai hayo.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Waitara ahoji bungeni mwarobaini mauaji katika mgodi Barick North Mara

Spread the loveMBUNGE wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara, ameitaka Serikali kutafuta...

error: Content is protected !!