Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Kikwete ahoji wanaume wamekwenda wapi
Elimu

Kikwete ahoji wanaume wamekwenda wapi

Jakaya Kikwete, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)
Spread the love

 

MKUU wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Jakaya Kikwete, ametaka utafiti ufanyike ili kujua kwa nini idadi ya wanaume katika kujiunga na taaluma kwenye chuo hicho imepungua, kwa kuwa katika udahili wake wa 2022 wanawake wameongezeka na kufikia asilimia 53. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Dk. Kikwete ambaye ni Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, ametoa kauli hiyo leo Jumatano, tarehe 30 Novemba 2022, katika mahafali ya 52 ya duru ya tano ya UDSM, baada ya Makamu Mkuu wa UDSM anayeshughulikia Taaluma, Prof. Boniventure Rutinwa, kusema wanafunzi 313 kati ya 640 (50%), wlaiopata ufadhili wa masomo kutoka Ufadhili wa Rais Samia Suluhu Hassan, wamejiunga na chuo hicho.

“Tuseme katika udahili mwaka huu asilimia 53 ni wanawake, sasa sijui watoto wa kiume wamekwenda wapi siku hizi, itabidi suala hili tukae na kulifanyia utafiuti huko waliokwenda sijui ni wapi,” amesema Dk. Kikwete.

Aidha, Dk. Kikwete ameponegza kitendo cha ongezeko la wanawake kujiunga chuoni hapo tena katika masomo ya sayansi, akisema huko nyuma ushiriki wao katika taaluma ulikuwa mdogo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu

Spread the loveSERIKALI imesema itaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ya elimu...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi

Spread the loveSERIKALI inakusudia kufanya mapitio katika mitaala na programu za vyuo...

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

error: Content is protected !!