Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Kikwete ahoji wanaume wamekwenda wapi
Elimu

Kikwete ahoji wanaume wamekwenda wapi

Jakaya Kikwete, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)
Spread the love

 

MKUU wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Jakaya Kikwete, ametaka utafiti ufanyike ili kujua kwa nini idadi ya wanaume katika kujiunga na taaluma kwenye chuo hicho imepungua, kwa kuwa katika udahili wake wa 2022 wanawake wameongezeka na kufikia asilimia 53. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Dk. Kikwete ambaye ni Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, ametoa kauli hiyo leo Jumatano, tarehe 30 Novemba 2022, katika mahafali ya 52 ya duru ya tano ya UDSM, baada ya Makamu Mkuu wa UDSM anayeshughulikia Taaluma, Prof. Boniventure Rutinwa, kusema wanafunzi 313 kati ya 640 (50%), wlaiopata ufadhili wa masomo kutoka Ufadhili wa Rais Samia Suluhu Hassan, wamejiunga na chuo hicho.

“Tuseme katika udahili mwaka huu asilimia 53 ni wanawake, sasa sijui watoto wa kiume wamekwenda wapi siku hizi, itabidi suala hili tukae na kulifanyia utafiuti huko waliokwenda sijui ni wapi,” amesema Dk. Kikwete.

Aidha, Dk. Kikwete ameponegza kitendo cha ongezeko la wanawake kujiunga chuoni hapo tena katika masomo ya sayansi, akisema huko nyuma ushiriki wao katika taaluma ulikuwa mdogo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!