CHAMA cha ACT-Wazalendo, kimeishauri Serikali iongeze shughuli za kiuchumi ili kukabiliana na changamoto za ongezeko la gharama za maisha, umasikini na ukosefu wa ajira. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Ushauri huo umetolewa na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, katika mahojiano yake na kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha ITV.
“Inapaswa ifanyike juhudi za makusudi kuongeza shughuli za kiuchumi, shughuli za uzalishaji hapa nchini na sekta ambayo inaweza kusaidia sana kuondokana na tatizo la ajira nchini ni sekta ya kilimo kuna kazi kubwa inapaswa kufanywa kuongeza shughuli za uzalishaji katika sekta ya kilimo, sio tu wazalishe lakini kuongeza thamani ya mazao,” amesema Zitto na kuongeza:
“Shughuli ya kilimo na mchakato wa kuongeza thamani ya mazao inaweza kutusaidia kukabiliana na matatizo matatu tunayokabiliana nayo, gharama ya maisha sababu sehemu kubwa ya gharama ni chakula ukiwa na cha kutosha unaukabili umasikini, ukishakuwa na shughuli za kiuchumi watu wanapata kipato na ukiwa na shughuli za kiuchumi unaajiri. Tunaishawishi Serikali itizame namna gani ya kupokea mtizamo huu ifanyie kazi ili kukabiliana na gharama za maisha na umasikini.”
Leave a comment