Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia aungana na viongozi 20 kuapishwa kwa Dk. Ruto
Habari za SiasaTangulizi

Samia aungana na viongozi 20 kuapishwa kwa Dk. Ruto

Spread the love

MACHO yote leo tarehe 13 Septemba, 2022 yanaelekezwa katika uwanja wa Kimataifa wa Moi, Kasarani Nairobi ambapo ndipo Dk. William Ruto ataapishwa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Kenya.

Dk. Ruto ataapishwa pamoja na Rigathi Gachagua, kama Rais na Naibu Rais mtawalia kwa mujibu wa sheria. Anaripoti Urumasalu Kisung’uda … (endelea).

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anaungana na baadhi ya marais wan chi mbalimbali Afrika na viongozi 20 kutoka pande tofauti za duniani, kushuhudiwa kuapishwa kwa Dk. Ruto ambaye pia alikuwa Naibu rais katika uongozi wa Uhuru Kenyatta.

Waliothibitisha kujumuika  katika hafla hiyo Rais Samia wengine ni Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Paul Kagame (Rwanda), Evariste Ndayishimiye wa Burundi, ambao ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Wengine ni Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC), Salva Kiir wa Sudan Kusini, Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe, Nana Akufo-Addo (Ghana), Lazarus Chikwera (Malawi) na Waziri Mkuu Ethiopia, Abiy Ahmed.

Hafla hiyo pia itahudhuriwa na Ismael Guelleh wa Djibouti, Hassan Sheikh (Somalia), Azali Asoumani (Comoros), Mfalme Mswati III (Eswatini), Wavel Ramkalawan (Sychelles), Filipe Nyusi wa Msumbiji, miongoni mwa wengine.

Rais anayeondoka, Uhuru Kenyatta atamkabidhi mikoba ya uongozi Dk. Ruto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!