MACHO yote leo tarehe 13 Septemba, 2022 yanaelekezwa katika uwanja wa Kimataifa wa Moi, Kasarani Nairobi ambapo ndipo Dk. William Ruto ataapishwa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Kenya.
Dk. Ruto ataapishwa pamoja na Rigathi Gachagua, kama Rais na Naibu Rais mtawalia kwa mujibu wa sheria. Anaripoti Urumasalu Kisung’uda … (endelea).
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anaungana na baadhi ya marais wan chi mbalimbali Afrika na viongozi 20 kutoka pande tofauti za duniani, kushuhudiwa kuapishwa kwa Dk. Ruto ambaye pia alikuwa Naibu rais katika uongozi wa Uhuru Kenyatta.
Waliothibitisha kujumuika katika hafla hiyo Rais Samia wengine ni Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Paul Kagame (Rwanda), Evariste Ndayishimiye wa Burundi, ambao ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Wengine ni Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC), Salva Kiir wa Sudan Kusini, Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe, Nana Akufo-Addo (Ghana), Lazarus Chikwera (Malawi) na Waziri Mkuu Ethiopia, Abiy Ahmed.
Hafla hiyo pia itahudhuriwa na Ismael Guelleh wa Djibouti, Hassan Sheikh (Somalia), Azali Asoumani (Comoros), Mfalme Mswati III (Eswatini), Wavel Ramkalawan (Sychelles), Filipe Nyusi wa Msumbiji, miongoni mwa wengine.
Rais anayeondoka, Uhuru Kenyatta atamkabidhi mikoba ya uongozi Dk. Ruto.
Leave a comment