SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Akson leo tarehe 13 Septemba, 2022 amemuapisha Tamima Haji Abass kuwa mbunge wa Bunge hilo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Tamima amekula kiapo hicho akichukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa Viti Maalum, Irene Ndyamkama aliyefariki dunia April 24,2022.
Kwa mujibu wa taratibu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) inatakiwa kupeleka jina la mtu kutoka ndani ya chama husika kuziba nafasi ya mbunge huyo aliyefariki.
Iwapo kama marehemu angekuwa mbunge wa kuchaguliwa kwa jimbo basi NEC ingetaka uchaguzi mdogo na vyama vingeshindanishwa.
Hata hivyo, katika uapisho wa leo hapakuwa na shamrashamra kama ilivyo kwa viapo vingine kwa wabunge.
Hadi sasa katika Bunge la 12, jumla ya wabunge sita wameshapoteza maisha, ikiwamo wabunge wawili wa viti maalumu ambao ni pamoja na Ndyamkama pamoja na aliyekuwa mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Manyara, Martha Umbura.
Leave a comment