Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia atuma salamu za rambirambi kifo cha Malkia Elizabeth II
Habari za SiasaKimataifa

Rais Samia atuma salamu za rambirambi kifo cha Malkia Elizabeth II

Malkia Elizabeth II
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha aliyekuwa kiongozi wa kimila nchini Uingereza, Malkia Elizabeth II. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia ametuma salamu hizo usiku wa kuamkia leo Ijumaa, tarehe 9 Septemba 2022, ikiwa ni saa kadhaa tangu familia ya kifalme itangaze kifo hicho kilichotokea jana mchana kwenye kasri la Balmoral, nchini Scotland, ambako marehemu Malkia Elizabeth alikuwa anapatiwa matibabu.

“Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha Malkia Elizabeth II. Kwa niaba ya Watanzania wote, natuma salamu za pole kwa Familia ya Kifalme @RoyalFamily na raia wote wa Uingereza. Malkia atakumbukwa duniani kote kama nguzo ya Amani, Umoja na Utulivu,” ameandika Rais Samia.

Malkia Elizabeth II aliitawala Uingereza kwa miaka 70, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 96, ameacha watoto wanne ambao ni Prince Charles, Princess Anne, Prince Andrew na Prince Edward.

Pia, Malkia Elizabeth ameacha wajukuu nane na vitukuu 12.
Kufuatia kifo chake, mtoto mkubwa wa Malkia Elizabeth, Prince Charles anarithi mikoba yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

error: Content is protected !!