Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waandamana kupinga mawakili wanaowatetea watuhumiwa wa kufuru Pakistani
Kimataifa

Waandamana kupinga mawakili wanaowatetea watuhumiwa wa kufuru Pakistani

Spread the love

MAKUNDI ya wafuasi wa Dini ya Kiislam na wafanyabiashara nchini Pakistani wameandamana kupinga watuhumiwa wa makosa ya kumdhihaki Mtume Muhammad (S.A.W) ‘kufuru’ jijini Khyber Pakhtunkhwa wasipate utetezi Mahakamani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Maandamano hayo yalifanyika wiki iliyopita katika soko kuu la wilaya ya Battagram na Ahle Sunnat Wal Jamaat, Jamaat-i-Islami, Jamiat Ulema-i-Islam-Fazl na wafanyabiashara.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari cha Dawn, miongoni mwa watuhumiwa wa makosa hayo ni Ofisa wa zamani wa Frontier Constabulary aliyekamatwa na kuzuiliwa chini ya kifungu cha 295-C cha Kanuni ya Adhabu ya Pakistani, chini ya kufuru.

Maandamano hayo yaliongozwa na rais wa mkoa wa ASWJ, Maulana Atta Mohammad Deshani, Katibu Mkuu wa JUI-F Maulana Faridudin, Jamaat-i-Islami Hafiz Rasheed Ahmad, viongozi wa wafanyabiashara Shah Hussain, Abdul Ghaffar Deshani na Katibu Mkuu wa zamani wa Chama cha Wanasheria wa Wilaya ya Battagram, Ziaullah Khan.

Walisema familia za watuhumiwa hazikuguswa na kwamba wameishinikiza Mahakama itoe idhabu ya mfano kwao.

Walisema iwapo polisi watatoa nafuu kwa washukiwa au kufanya uchunguzi mbovu, mawakili hao watawafikisha mahakamani.

Wanaharakati wanadai kuwa sheria hiyo inatumika vibaya ambapo inawaadhibu wachache.

Wanaeleza kuwa makundi ya walio wachache nchini Pakistani wanauawa kila mara na kufanyiwa ukatili wa kinyama kwa jina la kufuru, kuingia Uislamu na tofauti nyingine za kimadhehebu.

Kwa mujibu wa Tume ya Haki za Kibinadamu ya Pakistani, kesi za kukufuru si mpya nchini Pakistani. Takriban watu 585 waliwekwa kizuizini kwa tuhuma za kukufuru mwaka 2021, na idadi kubwa ya watu kutoka Punjab,

Pakistani ilitunga sheria za kukufuru baada ya kugawanyika na India mwaka 1947.

Hata hivyo, wakati wa utawala wa Jenerali Zia-ul Haq kati ya 1980 hadi 1986, vifungu kadhaa vilianzishwa ambavyo vilijumuisha kifungu cha kuadhibu kufuru dhidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) na adhabu ya jambo hilo ilikuwa kifo au kifungo kwa maisha.

Kulingana na takwimu za Tume ya Kitaifa ya Haki na Amani, Waislamu 776, Waahmadiyya 505, Wakristo 229 na Wahindu 30 wamefungwa chini ya sheria ya kukufuru kuanzia 1987 hadi 2018. (ANI).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!