Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko TPA yatangaza vipaumbele muhimu 5
Habari Mchanganyiko

TPA yatangaza vipaumbele muhimu 5

Spread the love

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari TPA imesema ujenzi wa miundombinu bora ya Bandari yenye mitambo ya kisasa  na sahihi ya kuhudumia meli na shehena ni mojawapo ya vipaumbele vitano ambavyo viko kwenye Mpango Mkakati wake wa Nne wa mwaka 2021/22-2025/26) wa mamlaka hiyo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma (endelea).

Hayo yameelezwa leo tarehe 13 Agosti, 2022 na Mkurugenzi wa Mipango, ubora na Uthibiti vihatarishi Dk. Boniface Nobeji alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mipango ya utekelezaji wa bajeti katika mwaka wa fedha 2022/23.

Aidha, amesema katika vipaumbele hivyo wanakusudia kuongeza shehena ya  nchi jirani  inayohudumiwa na bandari  za Tanzania na kuimarisha masuala ya ulinzi, usalama na mazingira katika utoaji wa huduma pamoja na kuzingatia miongozo ya kimataifa iliyoridhiwa na nchi.

Ameeleza kuwa vipaumbele hivyo vinatekelezwa na TPA kupitia Mipango na bajeti za kila mwaka.

Kuhusu shehena ya magari iliyohudumiwa katika Bandari ya Dar es Salaam kwa kipindi cha Julai 2021 hadi Juni 2022 ilikuwa 203,932 sawa na ongezeko la asilimia 38 ya magari 147,566 yaliyohudumiwa mwaka uliopita (Julai 2020 hadi Juni  2021).

Dk. Nobeji ameeleza kuwa ili kuendelea kutekeleza vipaumbele ilivyojiwekea, katika mwaka wa Fedha 2022/2023, TPA imetenga bajeti yake kwa malengo mbalimbali.

Ameyatenga malengo hayo kuwa  lengo la kwanza ni ukusanyaji wa mapato  Jumla ya sh.bilioni 1,224.405.

Pia matumizi ni sh.bilioni  866.051 na ziada ya sh.bilioni  358.354 kabla ya kodi.

Aidha, ameeleza kuwa bajeti ya miradi ya uwekezaji ikiwemo vitendea kazi ni sh.bilioni 762.606 na sh.bilioni 662.493  ni mapato ya ndani huku sh. bilion 100.112 ikitoka Serikalini (Ruzuku kwa utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!