Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Salman Rushdie apumulia mashine baada ya kuchomwa visu Marekani
KimataifaTangulizi

Salman Rushdie apumulia mashine baada ya kuchomwa visu Marekani

Spread the love

MWANDISHI wa habari mzaliwa wa Mumbai nchini India, Salman Rushdie, anapumulia mashine hospitalini baada ya jana tarehe 12 Agosti, 2022 kushambuliwa na visu. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Shambulio hilo lilitokea wakati akijitayarisha kutoa mhadhara jijini New York.

Mashahidi wanasema, mshambuliaji alipanda kwenye jukwaa ghafla na kumchoma visu mara kadhaa mwandishi huyo wa kitabu cha Aya za Shetani.

Wakala wake, Andrew Wylie, anasema Rushdie amejeruhiwa ini, mishipa ya damu na huenda akapoteza jicho moja.

Polisi inamshikilia mshambuliaji iliyemtaja kwa jina la Hadi Matar, mwenye umri wa miaka 24.

Rushdie, mwenye umri wa miaka 75, ameishi miaka mingi akiwa chini ya ulinzi wa polisi, kutokana na fatwa ya kifo dhidi yake iliyotolewa mwaka 1989 na kiongozi mkuu wa wakati huo wa Iran, Ayatullah Khomeini, baada ya mwandishi huyo kuandika riwaya yake ya nne, Aya za Shetani, ambayo inatajwa kuukashifu Uislamu.

Ingawa baadaye Iran ilijitenga na fatwa hiyo, lakini mwaka 2015, Wakfu wa 15 Khordad wa nchi hiyo ulitangaza zawadi ya dola milioni 3.3 kwa yeyote atakayemuuwa Rushdie.

Haijaweza kufahamika mara moja, mtekelezaji wa shambulio hilo alikuwa na malengo gani.     Salman Rushdie, mwandishi wa fasihi ambaye amekuwa akikabiliwa na kitisho cha kuuawa kutokana na uandishi wake; amekuwa akiishi kwa kutisho kwa karibu miongo mitatu sasa.

Mwandishi huyo wa fasihi alipangiwa kuzungumzia uhuru wa wasanii mbele ya hadhara ya mamia ya watu, alipovamiwa na mtu aliyefunika uso kwa barakowa.

Maafisa wa polisi waliokuwa katika ukumbi wa mkutano huo, waliingilia kati na kumtia mbaroni mshambuliaji.

Gavana wa New York, Kathy Hochul amelilaani shambulizi hilo, na amearifu kuwa Rushdie yuko hai na anaendelea kupatiwa matibabu.

Ama kuhusu hali ya afya yake, imearifiwa kuwa anapumua kwa kutumia mashine, na amepata majeraha mabaya usoni, shingoni na tumboni.

Polisi lakini wamesema bado hawajajua malengo ya mshambuliaji wake, wala kubainisha aina ya silaha aliyoitumia.

Hata msemaji wake amesema kupitia taarifa ya baruapepe kuwa mwandishi huyo anafanyiwa upasuaji bila kutoa maelezo zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!