Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kisa Ukraine, viongozi Ufaransa, Marekani Urusi watinga Afrika
Kimataifa

Kisa Ukraine, viongozi Ufaransa, Marekani Urusi watinga Afrika

Waziri wa Mambo ya nje wa Urusi, Sergey Lavrov akiwa na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni
Spread the love

VIONGOZI kutoka nchi za Ufaransa, Marekani na Urusi wanazuru bara la Afrika, katika kile kinachoelezwa ni kuyashawishi mataifa ya Afrika kuunga misimamo yao kuhusu vita vinavyoendelea nchini Ukraine. Anaripoti Juliana Assenga, (UDSM)… (endelea).

Hatua hii pia inaelezwa kama ushindani mkubwa wa mataifa hayo kuwahi kushuhudiwa barani Afrika, tangu wakati wa vita baridi.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amekuwa katika nchi za Cameroon, Benin na Guinea Bissau huku akiishtumu Urusi kama mkoloni anayesalia duniani.

Pia amewakosoa pia viongozi wa mataifa ya Afrika kwa kutoonesha msimamo thabiti wa kusimama na Ukraine na kuilaani Urusi kwa uvamizi unaoendelea.

Aidha, ameishutumu Urusi kwa kutumia vyombo vyake vya Habari kwa kueneza Habari za propaganda kuhusu vita vnavyoendelea nchini Ukraine.

Naye, Waziri wa Mambo ya nje wa Urusi, Sergey Lavrov ambaye amekuwa nchini Misri, Congo Brazavile, Uganda na Ethiopia ameyashtumu mataifa ya Magharibi kwa kuchochea mzozo kati yake na Ukraine.

Pia ameitetea nchi yake dhidi ya shutuma za kusababisha kupanda kwa gharama ya vyakula duniani.

Samantha Power, Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo nchini Marekani naye alikuwa nchini Kenya na Somalia wiki iliyopita.

Pia balozi wake kwenye Umoja wa Mataifa Linda Thomas-Greenfield, anatarajiwa kuzuru Ghana na Uganda wiki ijayo katika kile kinachoelezwa ni kuendeleza ushawishi kwa mataifa ya Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!