Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kisa Ukraine, viongozi Ufaransa, Marekani Urusi watinga Afrika
Kimataifa

Kisa Ukraine, viongozi Ufaransa, Marekani Urusi watinga Afrika

Waziri wa Mambo ya nje wa Urusi, Sergey Lavrov akiwa na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni
Spread the love

VIONGOZI kutoka nchi za Ufaransa, Marekani na Urusi wanazuru bara la Afrika, katika kile kinachoelezwa ni kuyashawishi mataifa ya Afrika kuunga misimamo yao kuhusu vita vinavyoendelea nchini Ukraine. Anaripoti Juliana Assenga, (UDSM)… (endelea).

Hatua hii pia inaelezwa kama ushindani mkubwa wa mataifa hayo kuwahi kushuhudiwa barani Afrika, tangu wakati wa vita baridi.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amekuwa katika nchi za Cameroon, Benin na Guinea Bissau huku akiishtumu Urusi kama mkoloni anayesalia duniani.

Pia amewakosoa pia viongozi wa mataifa ya Afrika kwa kutoonesha msimamo thabiti wa kusimama na Ukraine na kuilaani Urusi kwa uvamizi unaoendelea.

Aidha, ameishutumu Urusi kwa kutumia vyombo vyake vya Habari kwa kueneza Habari za propaganda kuhusu vita vnavyoendelea nchini Ukraine.

Naye, Waziri wa Mambo ya nje wa Urusi, Sergey Lavrov ambaye amekuwa nchini Misri, Congo Brazavile, Uganda na Ethiopia ameyashtumu mataifa ya Magharibi kwa kuchochea mzozo kati yake na Ukraine.

Pia ameitetea nchi yake dhidi ya shutuma za kusababisha kupanda kwa gharama ya vyakula duniani.

Samantha Power, Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo nchini Marekani naye alikuwa nchini Kenya na Somalia wiki iliyopita.

Pia balozi wake kwenye Umoja wa Mataifa Linda Thomas-Greenfield, anatarajiwa kuzuru Ghana na Uganda wiki ijayo katika kile kinachoelezwa ni kuendeleza ushawishi kwa mataifa ya Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!