Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mjadala sifa za waandishi wa habari waja
Habari Mchanganyiko

Mjadala sifa za waandishi wa habari waja

Spread the love

MWENYEKITI wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile, amesema wanaanda mjadala wa kitaifa kwa ajili ya kupata maoni na mapendekezo ya wadau kuhusu sifa na vigezo anavyopaswa kuwa navyo mwandishi wa habari, ikiwemo vya kitaaluma. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Balile ametoa taarifa hiyo leo Alhamisi, tarehe 2 Mei 2022, akizungumza katika mafunzo ya sheria za habari Tanzani kwa wanahabari, yaliyofanyika mtandaoni.

Mwenyekiti huyo wa TEF, alitoa kauli hiyo baada ya baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo yenye lengo la kuwawezesha wanahabari kuandika habari zinazohusu sheria za habari na mchakato wa marekebisho yake yanayoendelea sasa hivi, kuhoji vigezo sahihi vya mwandishi wa habari.

“Hilo swali limekuwa likiulizwa na watu mbalimbali, tumeona tuandae mjadala ambao uko wazi wa kitaifa ili kila mtu achangie kisha tukitoka tuwe tumekubaliana kama tunahitaji mtu mwenye sifa au mtu anayejua kusoma na kuandika awe mwanahabari au awe mtu aliyesomea taaluma,” amesema Balile.

Balile amesema, kwa sasa kuna mvutano kuhusu suala hilo, ambapo wako baadhi ya wadau wanapendekeza mwandishi wa habari awe mtu mwenye kipaji pasina kuisomea taaluma hiyo, wakati wengine wakikataa wakitaka mwanahabari awe ni mtu aliyesoma.

Katika hatua nyingine, Balile ameishauri Serikali, ifanye marekebisho katika kifungu cha tatu cha Sheria ya Huduma ya Habari ya 2016, ili kuondoa takwa lkinalomtambua mwandishi wa habari kuwa ni mtu mwenye taaluma na aliyepata leseni kutoka katika mamlaka husika.

Amesema, takwa hilo linazuia watu wa kawaida kufanya uandishi wa habari wa kijamii.

Hali kadhalika, Balile amesema TEF linaishauri Serikali ifanye marekebisho katika sheria hiyo, yatakayowezesha kila chombo cha habari kuwa na asilimia 30 ya waajiriwa wanawake, ili kupunguza changamoto ya uhaba wa wanahabari wanawake wanaoajiriwa katika tasnia ya habari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!