Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mfumo kuchakata majitaka wa DUWASA wamkosha katibu mkuu
Habari Mchanganyiko

Mfumo kuchakata majitaka wa DUWASA wamkosha katibu mkuu

KATIBU Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Mary Maganga (wanne kushoto) akisikiliza maelezo ya kuhusu mfumo wa majitaka unavyofanya kazi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), Mhandisi Aron Joseph (kushoto) ambao unachakata Majitaka kutoka hospitali ya Benjamini Mkapa jijini Dodoma leo 29.05.2022 ikiwani Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani.
Spread the love

KATIBU Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais nchini Tanzania, Mary Maganga ameipongeza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) kwa kuwa na mfumo bora na wa kisasa katika kuchakata majitaka ili kulinda mazingira. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Hayo aliyasema jana Jumapili tarehe 29 Mei 2022 wakati wa ziara yake katika eneo la mifumo ya kuchakata majitaka yanayotoka katika Hospitali ya Benjamini Mkapa jijini Dodoma ikiwa ni Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani.

KATIBU Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Mary Maganga (katikati) akisikiliza maelezo kuhusu mfumo wa majitaka unavyofanya kazi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), Mhandisi Aron Joseph (kushoto) ambao unachakata Majitaka kutoka hospitali ya Benjamini Mkapa jijini Dodoma jana tarehe 29 Mei, 2022 ikiwani Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani.

“Hongereni sana kwa mifumo hii mizuri, afadhali na sisi tuna kitu kizuri ambacho tunaweza kujivunia katika suala la uchakataji wa majitaka hapa Dodoma” alisema Katibu Mkuu Maganga.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma, Mhandisi Aron Joseph alisema mfumo huu wa majitaka unafanya kazi kwa ufasaha mkubwa katika kuondoa takasumu pamoja na kemikali nyingine zinazoweza kuathiri mazingira.

Mifumo hiyo ya kuchakata Majitaka katika eneo la Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) inasimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma na inahudumia chuo pamoja na hospitali.

KATIBU Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Mary Maganga akipanda mti wa mparachichi katika eneo la mifumo ya kuchakata majitaka inayoendeshwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) baada ya kuikagua jijini Dodoma jana tarehe 29 Mei, 2022 ikiwani Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani. Watatu kulia ni Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), Mhandisi Aron Joseph.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Majitaka na Mazingira DUWASA, Mhandisi Daniel Mgunda alisema changamoto kubwa wanayokutana nayo ni matumizi yasiyo sahihi kwa watumiaji.

“Watu wengi hawajui matumizi sahihi ya mfumo wa majitaka hivyo wanatupa vitu vigumu kama chupa, nguo, vitambaa na nepi katika mfumo na kusababisha kuziba mara kwa mara,” alisema Mgunda.

Pia, alisema kumekuwa na wizi mkubwa sana wa mifuniko kwa watu wasiokuwa wema ambao mpaka sasa tumekuwa tukipambana nao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!